Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Huu ndiyo Mpango wa serikali katika kuinua michezo

Thursday , 8th Apr , 2021

Mkurugenzi wa michezo nchini, Yusuph Singo ameiambia EATV kuwa, serikali imeadhimiria kushiriki katika mageuzi ya michezo kwa kujenga vituo mbali mbali vya michezo nchini ili kuibua na kukuza vipaji.

Mkurugenzi wa Michezo nchini, Yusuph Singo.

Singo amesema tayari Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo imefanya mkutano kwa pamoja na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia pamoja na Wizara ya ofisi ya Rais tawala za mikoa na serikali za mitaa 'TAMISEMI' na kukubaliana kufungua shule mbili za kukuzia vipaji kila mkoa.

“Mwaka huu tumeanza mkakati wa kufungua 'Center of sports excellence chuo cha maendeleo ya michezo Malya (Mwanza) kwa maana ya kwamba tutahifadhi vipaji, tutavitia vipaji, tutavitafuta vipaji, tutakuwa tunavikuza  pale kama serikali kutoa mfano ili kuhakikisha tunafanya vizuri katika michezo”.

Singo akasisitiza kuwa “Serikali imedhamiria, Serikali tayari imetenga fedha kidogo kwa ajili ya kuanzisha taifa cup ya vijana umri wa miaka 15 hadi 17 tutaianza mwaka huu Mungu akipenda”

Katika kufanikisha mageuzi hayo ya michezo nchini, Singo ametoa wito kwa wazazi kuunga mkono juhudi hizo kwa kuhakikisha wana wasaidia watoto wao kujiunga kwenye vituo vya michezo.

“Wazazi watambue kwamba, Mungu ameumba binadamu na amewapa vipaji mbalimbali, wapo waliopewa vipaji vya kusoma, wapo waliopewa vipaji vyote na wapo waliopewa vipaji vya kufanya michezo, wazazi tuwaunge mkono watoto wetu kwenye vipaji ambavyo wanavyo”.

“Michezo sasa hivi ni ajira ina lipa pesa nyingi sana hakuna watu wanaolipwa pesa nyingi kama watu wa michezo. Kwahiyo wawe sehemu ya kuwanunga mkono watoto wetu ili wajiunge na vituo vya michezo ili waweze kuja kuwa wachezaji wazuri na kujipatia ajira”.

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea

Bashiri Mohamed (35) Mwenye Koti Jeusi akiwa anafikishwa Mahakamani Ilemela, Jijini Mwanza

Aliyezini na binti yake apandishwa kizimbani