.jpg?itok=o2DWR1h-×tamp=1665499006)
Ajali Rungwe Mbeya
Kwa mujibu wa Mkuu wa Wilaya ya Rungwe, Dk Vincent Anney, ajali hiyo imetokea leo Oktoba 11, 2022 majira ya asubuhi katika kitongoji cha Kanyegere, Kijiji cha Ibula, Kata ya Kiwira, Wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya.
Dk Anney amesema kwamba, miongoni mwa watu waliopoteza maisha ni pamoja na dereva wa Coaster iliyokuwa ikisafirisha maiti kutoka Dodoma, kwenda Kyela.