Monday , 17th Oct , 2022

Kufuatia kuwepo kwa ongezeko la matukio ya ulawiti na ubakaji kwa watoto Jeshi la Polisi wilaya ya kiPolisi Nyamwaga Wilayani Tarime Mkoani Mara limewasihi wazazi na walezi kujenga mazoea ya kuongea na watoto pamoja na kuwakagua watoto wao ili kuweza kubaini vitendo vya ukatili

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa kituo cha Polisi wilaya ya Kipolisi Nyamwaga SP Fatma Mbwana katika uzinduzi wa tamasha la michezo lilolenga kutoa elimu juu ya madhara ya ukatili kwa watoto na wanawake wilayani hapo.

Nao baadhi ya wananchi wanazungumzia Suala la elimu kuendelea kutolewa kwenye jamii ili kutokomeza  vitendo vya ukatili  ambavyo vinaonekana kushamiri kwa siku hizi za karibuni kote nchini.