Monday , 28th Nov , 2022

Mahakama nchini Comoro imemuhukumu adhabu ya kifungo cha maisha jela rais wa zamani wan chi hiyo  Ahmed Abdallah Sambi kutokana na makosa ya a uhaini.

Kiongozi wa huyo wa zamani alipatikana na hatia ya kuuza pasipoti kwa watu wasio na utaifa wanaoishi katika Ghuba na alikuwa ameshtakiwa kwa ubadhirifu wa mamilioni ya dola.

Akitolea mfano wa kesi isiyo ya haki, Sambi mwenye umri wa miaka 64, alikataa kuhudhuria vikao hivyo katika Mahakama ya Usalama wa Taifa ambayo uamuzi wake hauwezi kukatiwa rufaa.

Sambi  ambaye ni mpinzani mkuu wa Rais wa Comoro Azali Assoumani  alikuwa tayari amekaa gerezani kwa miaka minne kabla ya kukabiliwa na kesi.