Mkuu wa wilaya hiyo, Thomas Bakenge amesema kuwa idadi ya waliokufa imefika 401, na ilitarajiwa kuongezeka kwa sababu shughuli ya kuwatafuta wahanga imekuwa ikiendelea na Kulingana na taarifa kutoka eneo hilo, miili ipatayo 300 ya wahanga hao tayari imezikwa
Mvua kubwa ilianza kunyesha wilayani Kalehe jioni ya Alhamisi iliyopita, ikaifanya mito kuvunja kingo zake na kuzisomba nyumba nyingi katika vijiji vya Bushushu na Nyamukubi, na kusababisha hasara kubwa ya maisha na mali.
Afisa wa asasi ya kiraia katika eneo hilo, Delphin Birimbi amesema uharibifu wa miundombnu uliotokana na mafuriko hayo unakwamisha operesheni za uokozi.