Tuesday , 20th May , 2025

Msanii wa muziki wa singeli Tanzania ametupa lawama za kuibiwa wimbo na msanii D voice ambapo kwa mujibu wake ni kuwa D voice ameuvujisha wimbo huo kwa Jux baada ya Meja kumsikilizisha kama mdogo wake.

Pichani Jux,Meja Kunta na D Voice

Meja ameshare nyimbo zote katika ukurasa wake wa instagram huku akitupa lawama zote kwa msanii D voice akidai kuwa hakutegemea kama mdogo wake huyo anaweza kumfanyia hivyo licha ya wawili hao kuwa watu wa karibu kuanzia kwa wazazi wao

Kupitia ukurasa wa Instagram Msanii Meja Ameandika...............''D voice Inawezekana Kwenye Hii Game Nikawa Mtu Wa Kwanza Mwenye Ukaribu Nawewe Kutokana Na Ukaribu Wa Familia Zetu.Inawezekana Nikawa Ndie Mtu Niliekufungulia Milango Mingi Kwenye Maisha Yako Tulipofanya Wimbo Wa Pamoja Ulifanya Vizuri Sana

 

Hii Inaonyesha Kiasi Gani Wewe Ni Mdogo Wangu Wa Rohoni Kabisa Nina Mapenzi Makubwa Na Wewe Ila Hiki Unachofanya Kina Tafsiri Mbili Dharau,Kunitumia, Tunawasiliana Kila siku Tunakutana Kila Siku Sidhani Kama Natakiwa Kulipwa Hiki''