Kagoma, Oura na Kibabage wapo fiti kuivaa Yanga
Meneja wa Habari wa klabu ya Simba, Ahmed Ally amethitibitisha kuwa wachezaji watatu wa klabu hiyo Anicet Oura, Nickson Kibabage na Yusuph Kagoma ambao walitolewa kwenye fainali ya Kombe la Muungano 2026 dhidi ya Yanga SC wapo vizuri kuelekea Dabi ya Mei 3, 2026 kwenye ligi kuu bara.

