Bw. Altemius Millinga
Hayo yameelezwa leo Jijini Dar es Salaam na Makamu Mwenyekiti wa Muungano wa Taasisi za Kifedha unaojulikana kwa kifupi kama TAMFI, Bw. Altemius Millinga, wakati akizungumzia mkutano unaondelea wa wanachama wa mtandao huo, wanajadili mpangilio bora wa shughuli za asasi za kifedha kwenye sheria ya usimamizi wa asasi za kifedha ambayo serikali inakusudia kuja nayo hivi karibuni.
Bw. Millinga amesema idadi ndogo yas watumiaji wa huduma za kifedha zinazotolewa na mabenki ndiyo chanzo cha riba kubwa na kwamba hali inaweza kuwa bora iwapo watumiaji wa huduma za kifedha itaongezeka kama ilivyokuwa kwenye sekta ya mawasiliano ya simu za mkononi na intaneti.