
Bashiru Ally ametoa kauli hiyo wakati akizungumza kwenye mkutano wake na wanachama wa chama hicho Kigoma Mjini, ambapo amesema wapinzani wao wajiandae kushindwa.
Bashiru amesema kuwa "CCM tukishindwa tukubali tumeshindwa, tuliposhindwa Kigoma Mjini tulikubali, na wajifunze kuwa aliyeshindwa akirudi awamu ya pili akakung'oa na yeye akubali"
"Niwaambie Kigoma Mjini na Kigoma nzima ambapo hatukushinda, tumejipanga kushinda, wajiandae kushindwa" amesema Bashiru
#VIDEO Katibu wa @ccm_tanzania Bashiru Ally amevitaka vyama vya upinzani kujiandaa kukubali kushindwa kama ambavyo CCM ilikubali katika baadhi ya majimbo ikiwemo jimbo la Kigoma Mjini, hivyo nao wanatakiwa kuiga mfano wa CCM na waanze mapema kujiandaa kukubali kushindwa. pic.twitter.com/cK6brtjTEp
— East Africa TV (@eastafricatv) January 18, 2020