
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan
Kauli hiyo ameitoa hii leo Mei Mosi, 2022, wakati akizungumza na wafanyakazi pamoja na wananchi walijitokeza mkoani Dodoma wakati wa maadhimisho ya siku ya wafanyakazi dunia inayojulikana kama #MeiMosiDay
"Ulezi wa Mama unaendelea, yale mambo mbalimbali tuliyoyafanya mwaka huu kupunguza kodi hiki na kile tutaendelea kuyafanya, jambo letu lipo (Mshahara) si kwa kiwango kilichosemwa na TUCTA kwa sababu mnajua hali ya uchumi wa nchi yetu na Dunia hali si nzuri sana, nimeagiza jambo liwepo, mahesabu yanaendelea, tutajua lipo kwa kiasi gani," amesema Rais Samia