Takwimu hizo zimetolewa na Katibu tawala Mkoa Hassan Rugwa katika kikao kazi cha tathmini ya mwendo wa elimu.
Imeelezwa kuwa mkoa wa Katavi kwa upande wa elimu msingi unakabiliwa na changamoto ya upungufu wa madarasa zaidi ya 3800 Hali inayopelekea baadhi ya shule kukaa wanafunzi zaidi ya 200 kwa darasa Moja.
Nao baadhi ya waalimu wamesema utoro unatokana na shule kuwa mbali na makazi na msongamano wa wanafunzi darasani pia unasababisha ufaulu kushuka hasa kwenye mitihani ya kitaifa.

