
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Kamishna Msaidizi wa Polisi Benjamin Kuzaga, amesema watuhumiwa hao wamekamatwa eneo la Kijiji cha Songwe, Kata ya Bonde la Songwe wilayani Mbeya baada ya Jeshi la Polisi kupata taarifa za siri na kuweka mtego uliofanikisha kuwatia mbaroni.
Nae Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA, Mkoa wa Mbeya, Musibu Shaban amesema bidhaa zilizokamatwa ni za magendo na kwamba taratibu za kisheria zitafuatwa.