Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mary Masanja
Hayo yamesemwa leo Bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mary Masanja wakati akijibu swali la Mbunge wa Malinyi Antipas Mgungusi, aliyetaka kujua lini Jeshi la Uhifadhi litapata Kamishna Jenerali ili kukamilisha muundo wa kijeshi na kuleta muunganiko katika divisheni ya NCAA, TANAPA,TAWA na TFS.
"Taasisi hizi zina majukumu tofauti kwa mfano Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori (TAWA) na Wakala ya Huduma za Misitu Tanzania (TFS) zinaruhusu uvunaji na uwindaji wa kitalii, tofauti na Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) na Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro (NCAA)," amesema naibu waziri Masanja
Amefafanua kuwa endapo kutabainika kuwa na changamoto katika utekelezaji wa mfumo huo, serikali itafanya marejeo ya sheria ya wanyamapori ili kuwezesha kuwa na Kamishna Jenerali wa Jeshi la Uhifadhi wa Wanyamapori na Misitu.