Makaburi yabomolewa, baadhi ya viungo vyaibiwa
Mkuu wa wilaya ya Magu mkoani Mwanza Salum Kali, amesema bado wanaendelea kuwatafuta waliobomoa na kuiba baadhi ya vitu kama misalaba na baadhi ya viungo vya miili ya watu waliozikwa kwenye makaburi ya wilaya hiyo ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao.

