Together Tunawakilisha
Home

YOU ARE NOT LOGGED IN
  • Login
  • or
  • Sign Up
  • Dashboard
  • Logout
  • Home
  • Shows
  • News
    • Currrent Affairs
    • Entertainment
    • Sport
    • Business
    • Life & Style
  • Gallery
  • Schedule
  • Namthamini
  • Wanafunzi wa shule ya sekondari Kyanyari wakipokea taulo za kike

    Wanafunzi wa kike 800 wapatiwa taulo za kike Mara
    Wilaya mbili za Musoma na Butiama kila wilaya ilipokea taulo za kike 400
  • Balozi wa kampeni ya Namthamini, Justine Kessy akizungumza na Meneja Rasilimali watu wa ITV, Bi. Hellen Elipokea wa katikati.

    ITV wachangia Namthamini pakiti 1200
    Ambazo zinaweza kuwasaidia wanafunzi 100 kwa mwaka mzima
  • Balozi wa kampeni ya Namthamini, Justine Kessy akipokea taulo za kike kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Luna Pads, Luna Kikuchi.

    Luna Pads wamthamini mtoto wa kike
    Wamechangia taulo za kike pakiti 50 ili kumbakisha binti shuleni
  • Mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Mbambi akipokea zawadi ya t-shirt ya Namthamini.

    Namthamini 2022 wanafunzi wamepata zawadi kibao
    Wamepatiwa taulo za kike na elimu ya hedhi salama
  • Namthamini 2022 wanafunzi wamepata zawadi kibao
    Wamepatiwa taulo za kike na elimu ya hedhi salama

Wasichana

kutoka mikoa zaidi ya 15 Tanzania wamenufaika

Msaada wa Pesa

Changia kiasi chochote cha pesa
5,000/=
(Je wajua kwa TZS 5,000/= inamweka mtoto wa kike shule mwezi mzima?)
Changia (Donate)
Toa mchango wako wa Fedha kwa njia zifuatazo
1
Bank
Akaunti Namba: 015043198200
Jina la Account: Namthamini
Jina la Benki: CRDB
2
MPESA
Unaweza kuchangia kwa namba ya malipo 5999900
jina East Africa Television
Kwa mawasiliano zaidi piga 0787 633 313

Changia Pedi

Changia pedi kumsaidia binti mmoja kwa mwaka.
Changia (Donate)
Wasilisha mchango wako wa PEDI
Ofisi za East Africa Television na East Africa Radio, Mikocheni, Dar es salaam.
Kwa mawasiliano zaidi piga 0787 633 313
Habari

Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP Abdiel Mengi akiongoza matembezi ya hisani yenye lengo la kuhamasisha uchangiaji wa taulo za kike kwaajili ya wanafunzi shuleni.

Matembezi ya kuhamasisha hedhi salama mashuleni

Wananchi mbalimbali wamejitokeza kushiriki matembezi ya hisani ya kampeni ya Namthamini...

Soma zaidi

Matembezi ya kuhamasisha hedhi salama mashuleni

Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP Abdiel Mengi akiongoza matembezi ya hisani yenye lengo la kuhamasisha uchangiaji wa taulo za kike kwaajili ya wanafunzi shuleni.

Matembezi hayo ambayo yameandaliwa na East Africa Television na East Africa Radio kupitia kampeni ya Namthamini Nasimama Naye yamefanyika leo Agosti 25, Makao makuu ya East Africa Television na East Africa Radio Mikocheni, jijini Dar es Salaam ambapo wadau wametoa wito kwa jamii kuchangia na kushiriki masuala ya kijamii.

Wakizungumza baada ya matembezi hayo wadau mbalimbali ikiwemo Mamlaka ya Elimu Tanzania TEA wameeleza kuhusu umuhimu wa jamii kushiriki kuchangia upatikanaji wa taulo za kike kwa wanafunzi nchini.

Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP Abdiel Mengi akiongoza matembezi ya hisani yenye lengo la kuhamasisha uchangiaji wa taulo za kike kwaajili ya wanafunzi shuleni.

''Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA), iliona kuna umuhimu wa kushirikiana na Television na East Africa Radio, kuhakikisha inaunga mkono juhudi zao za kumuwezesha binti wa kitanzania aliyekuwa anakosea siku 5 mpaka 7 za masomo kwa sababu ya hedhi , na sisi TEA, tutahakikisha changamoto hiyo inatatuliwa kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa Elimu'', Mwanaisha Chambega - Mkurugenzi huduma za Taasisi TEA

''Katika Shule zitakazopata nafasi zinapata Choo bora vitakavyowawezesha mabinti kubadilisha taulo zao wawapo shuleni bila kukutana na changamoto ya kimazingira'', Eliminatha Pascal - Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Amref Tanzania.

Washiriki mbalimbali wa matembezi ya hisani ya Namthamini

"Sidi Singida Sunflowers tunaahidi kuchangia Taulo za kike kwa shule ambazo zitachaguliwa kutembelewa na kampeni hii kabambe ya kumuwezesha mtoto wa kike ahudhurie masomo yake bila changamoto", Buruan Salim - Mkurugenzi Singida Rafiki Sunflower.

"Total energies tutashirikiana na TEA, kuchangia taulo za kike kwenye shule zote zitakazochaguliwa na kutembeelewa na tutahakikisha mtoto wa kike anabaki kwenye mazingira salama", Faith Mfugale - Mwakilishi Total Energies.

"Kupitia Kampeni hii tutahakikisha kila shule inapata maji safi na salama pamoja na miundombinu yake", Veronica Ussiri - Mwakilishi Sayari Safi.

Washiriki mbalimbali wa matembezi ya hisani ya Namthamini

"Shule zote zitakazotembelewa tutaweka wataalam wetu ka ajili ya kutoa Elimu ya matumizi sahihi ya taulo nza kike na Elimu kuhusu hedhi salama", Japhet Mswaki - Mwakilishi Tanzania save the community.

"Tutatoa mchango wetu wa hali na mali kwa kushirikiana na Television na East Africa Radio, kuhakikisha kamopeni hii inafanikiwa kwa asilimia zote", Kassim Juma - Mwakilishi Hisense.

"Nimeona nichangie taulo hizi ili watoto wetu waweze kubaki shuleni kwa siku za hedhi", Joseph Abdallah-Mwenyekiti Mtaa wa Jitegemee mabibo.

Washiriki mbalimbali wa matembezi ya hisani ya Namthamini

"Tumeshiriki katika kutoa huduma ya kwanza kwenye matembezi haya kama kuta morali kwa jamii kuthamini mchango wa mtoto wa kike", Junior Mshitu - Mwakilishi THMS

"Nimetengeneza madirisha ya chuma kwa ajili ya vyoo vitakavyojengwa kwa ajili ya wanafunzi kujitiri", Saidi Abeid - Fundi Kuchomelea.

"Tuliona vema kuungana na wenzetu wa EATV kutoa elimu kwa pamoja kwani hakuna mama ambaye hajapitia kuwa binti na sisi tunaungana nao kuhamasisha jamii kuchangia taulo za kike", Agaton Kigawa - Mwenyekiti Riverside Jogging.

 
 
 
 

View this post on Instagram
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 

A post shared by EastAfricaTV (EATV) (@eastafricatv)

"Wote tunajua dada zetu kuwa wanaingia kwenye siku zao naunga mkono zoezi hili kwa ajili ya dada zetu", Kasius Ndyamkama - Kiongozi Muongoz Fitnes.

Nini hasa kampeni hii imelenga? "Huu ni msimu wa nane wa kampeni hii na tumelenga kusaidia watoto wa kike mashuleni kupata taulo za kike ili waweze kusalia madarasani inapofika kipindi cha hedhi", Najma Paul.

 
 
 
 

View this post on Instagram
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 

A post shared by EastAfricaTV (EATV) (@eastafricatv)

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP Abdiel Mengi ameeleza jinsi ambavyo IPP imekuwa mstari wa mbele kuthamini mchango wa mwanamke kwenye jamii huku akitoa wito kwa wadau wengine kujitokeza kusaidia kufikiwa kwa malengo ya kampeni hiyo.

Balozi wa kampeni ya Namthamini, Justine Kessy akikabidhi taulo za kike kwa Mkuu wa Wilaya ya Hanang, Janeth Mayanja.

EATV watoa msaada kwa wahanga wa Katesh

East Africa TV na East Africa Radio kupitia kampeni ya Namthamini tumekabidhi taulo za kike...

Soma zaidi

EATV watoa msaada kwa wahanga wa Katesh

Balozi wa kampeni ya Namthamini, Justine Kessy akikabidhi taulo za kike kwa Mkuu wa Wilaya ya Hanang, Janeth Mayanja.

Balozi wa kampeni ya Namthamini Justine Kessy amekabidhi taulo za kike zipatazo pisi 2632 kwa Mkuu wa Wilaya ya Hanang, Janeth Mayanja ambazo zitaweza kuwasaidia wanawake na mabinti zaidi ya 200 kwa kipindi cha mwaka mzima.

Balozi wa kampeni ya Namthamini, Justine Kessy akikabidhi taulo za kike kwa mwanafunzi wa shule ya Sekondari Kyanyari iliyopo Butiama, Mara

Wanafunzi 872 Mara wapatiwa taulo za kike

Siku ya jana Novemba 08, 2023 kampeni ya Namthamini ilifika katika mkoa wa Mara na kugawa taulo...

Soma zaidi

Wanafunzi 872 Mara wapatiwa taulo za kike

Balozi wa kampeni ya Namthamini, Justine Kessy akikabidhi taulo za kike kwa mwanafunzi wa shule ya Sekondari Kyanyari iliyopo Butiama, Mara

Kampeni ya Namthamini ilianza na wanafunzi wa shule ya msingi ya watoto wenye ulemavu Mwisenge iliyopo wilaya ya Musoma mkoani Mara ambao walipatiwa taulo za kike ambazo zitaweza kuwasadia wanafunzi 400 wa kike kwa mwaka mzima.

Kisha ikaelekea katika wilaya ya Butiama katika shule ya Sekondari Kyanyari ambapo zilitolewa taulo za kike zenye uwezo wa kuwasaidia wanafunzi 400 kwa kipindi cha mwaka mzima.

Mbali na kupatiwa taulo za kike wanafunzi wa shule hiyo walipatiwa elimu ya hedhi salama na kujengewa uwezo wa kujiamini wanapokuwa kwenye kipindi cha hedhi.

 
 
 
 

View this post on Instagram
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 

A post shared by EastAfricaTV (EATV) (@eastafricatv)

Lucia Masinde mwanafunzi wa kidato cha tatu shule ya Sekondari Kyanyari anasema kabla ya kupata elimu ya hedhi salama kupitia kampeni ya Namthamini wanafunzi walikuwa hawashirikiani wanapokuwa kwenye kipindi cha hedhi na wanafunzi wengine walikuwa wanatumia vitambaa kujistiri kutokana na kukosa uwezo wa kununua pedi.

  • Tazama zaidi

Namthamini

  • English
Kampeni
Namthamini

Mwaka 2017 East Africa Television LTD ilianzisha kampeni ya kuchangisha taulo za kike kwa wanafunzi wenye uhitaji shuleni. 

Kampeni hii ilikuja baada ya tafiti kuonesha kuwa wasichana wengi hupata changamoto katika siku zao za hedhi kwa kushindwa kununua taulo za kike hivyo kupelekea kukosa masomo shuleni kwa takribani siku 3 mpaka 7 kwa mwezi za masomo. 

2024 ni mwaka wa saba (8) tangu kuanzishwa kwa mradi huu, tukishiriana na Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) lengo kuu likiwa ni kuhakikisha watoto wa kike wanapata sio tu taulo za kike lakini pia wanakuwa na vyoo vizuri na maji safi mashuleni ili wabaki salama katika siku zao za hedhi.

Mwaka huu 2024, kampeni hii ina lengo la kufikia watoto wa kike 10,000 katika mikoa mbali mbali nchini Tanzania.

Lengo la Kampeni
Lengo letu kuu ni kumsaidia msichana huyu kwa kumpatia taulo salama na kuhakikisha hakosi tena masomo yake na anafikia ndoto zake.

'Unapomuinua mtoto mmoja wa kike, umeinua jamii nzima' 
#Namthamini 
#NasimamaNaye

Shule Nufaika
Arusha
Shule ya Sekondari Arusha
Arusha
Shule ya Sekondari Arusha
Arusha
Shule ya Sekondari Kinana
Arusha
Shule ya Sekondari Muriet
Arusha
Shule ya Sekondari Musa
Arusha
Shule ya Sekondari Ngarenaro
Bukoba
Shule ya Sekondari Izimbya
Bukoba
Shule ya Sekondari Ruhunga
Dar es salaam
Shule ya Msingi Rahaleo
Dar es salaam
Shule ya Msingi Tuliani
Dar es salaam
Shule ya Msingi Uhuru Mchanganyiko
Dar es salaam
Shule ya Sekondari Abdu Jumbe
Dar es salaam
Shule ya Sekondari Buza
Dar es salaam
Shule ya Sekondari Jangwani
Dar es salaam
Shule ya Sekondari Kibugumo
Dar es salaam
Shule ya Sekondari Kidete
Dar es salaam
Shule ya Sekondari Kisota
Dar es salaam
Shule ya Sekondari Kisutu
Dar es salaam
Shule ya Sekondari Maendeleo
Dar es salaam
Shule ya Sekondari Minazini
Dar es salaam
Shule ya Sekondari Tungi
Dar es salaam
Shule ya Sekondari Turiani
Dar es salaam
Shule ya Sekondari Twiga
Dodoma
Shule ya Sekondari Hombolo
Dodoma
Shule ya Sekondari Kikombo
Dodoma
Shule ya Sekondari Msalato
Iringa
Shule ya Sekondari Lukosi
Iringa
Shule ya Sekondari Mazombe
Iringa
Shule ya Sekondari Nyalumbu
Kigoma
Shule ya Sekondari Bogwe
Kigoma
Shule ya Sekondari Katubuka
Kigoma
Shule ya Sekondari Kigoma Grand
Kigoma
Shule ya Sekondari Mlole
Kigoma
Shule ya Sekondari Murubona
Kigoma
Shule ya Sekondari Mwananchi
Lindi
Shule ya Sekondari Mchinga
Lindi
Shule ya Sekondari Ngongo
Manyara
Shule ya Sekondari Simbay
Manyara
Shule ya Sekondari Sumaye
Mara
Shule ya Msingi Mwisenge
Mara
Shule ya Sekondari Kyanyari
Mbeya
Shule ya Sekondari Busokelo
Mbeya
Shule ya Sekondari Garijembe
Mbeya
Shule ya Sekondari Kalonge
Mbeya
Shule ya Sekondari Maziwa
Mbeya
Shule ya Sekondari Nsenga
Mbeya
Shule ya Sekondari Stellafam
Mbeya
Shule ya Sekondari Usongwe
Mtwara
Shule ya Sekondari Chiungutwa
Mtwara
Shule ya Sekondari Lukuledi
Mtwara
Shule ya Sekondari Mangamba
Mtwara
Shule ya Sekondari Masasi
Mtwara
Shule ya Sekondari Mikindani
Mtwara
Shule ya Sekondari Mitengo
Mtwara
Shule ya Sekondari Naliendele
Mtwara
Shule ya Sekondari Nanyumbu
Mtwara
Shule ya Sekondari Napacho
Njombe
Shule ya Sekondari Iwawa
Njombe
Shule ya Sekondari Kitulo
Njombe
Shule ya Sekondari Mabatini
Njombe
Shule ya Sekondari Mavala
Njombe
Shule ya Sekondari Mchuchuma
Pwani
Shule ya Sekondari Dunda
Pwani
Shule ya Sekondari Kibuta
Pwani
Shule ya Sekondari Maneromango
Pwani
Shule ya Sekondari Matimbwa
Ruvuma
Shule ya Sekondari Luwawasa
Ruvuma
Shule ya Sekondari Manyanya
Ruvuma
Shule ya Sekondari Mashujaa
Ruvuma
Shule ya Sekondari Mbambi
Ruvuma
Shule ya Sekondari Mbinga
Shinyanga
Shule ya Sekondari Kishapu
Shinyanga
Shule ya Sekondari Mwataga
Shinyanga
Shule ya Sekondari Samuye
Shinyanga
Shule ya Sekondari Tinde
Simiyu
Shule ya Sekondari Badi
Simiyu
Shule ya Sekondari Binza
Simiyu
Shule ya Sekondari Kidinda
Simiyu
Shule ya Sekondari Somanda
Singida
Shule ya Sekondari Gunda
Singida
Shule ya Sekondari Ntuntu
Tabora
Shule ya Sekondari Idete
Tabora
Shule ya Sekondari Ikomwa
Tabora
Shule ya sekondari Ndono
Tabora
Shule ya Sekondari Tura
Tanga
Shule ya Sekondari Korogwe
Tanga
Shule ya Sekondari Kwamatuku
Tanga
Shule ya Sekondari Kwedzinga
Tanga
Shule ya Sekondari Segera
Yaliyosemwa
  • "Rotary tulianzisha mradi wa kuwawesha mabinti katika masuala ya hedhi, club zote nchini zinaelimisha wavulana kwa wasichana kuhusu hedhi salama kwa kushirikiana na wadau wetu kama kampeni ya Namthamini"
    Aisha Sykes
    Rotary Oysterbay
    Rais wa Rotary Oysterbay
  • “Nawashukuru sana kwa namna ambavyo mnahudumia jamii ya watoto wa Tanzania, asanteni kwa huduma mnayoifanya kwa watoto wetu”
    Rosalia Mwita
    Twiga Sekondari
    Mkuu wa Shule
  • ''Nawapongeza East Africa TV na Radio kwa jitihada zao katika Kampeni hii na mimi na naungana nao, tuendelee kuwa pamoja katika hili ili tuweze kuwasaidia mabinti zetu na tuzalishe viongozi wa kike wengine wazuri katika siku za baadae'' - Mh. Fatma Nyangasa
    Fatma Nyangasa
    Wilaya ya Kigamboni
    Mkuu wa Wilaya
  • "Kuhusu kampeni ya #Namthamini mimi mwenyewe nimeshiriki kuongea na wazazi kuhusu umuhimu wa kuhakikisha mtoto wa kike anapata elimu na anatimiza ndoto zake".
    Thobias Andengenye
    Kigoma
    Mkuu wa Mkoa wa Kigoma
  • 'Nawashukuru kwa kuja na wazo hili la kampeni ya #Namthamini hili litamsaidia mtoto wa kike kuwa huru na kuondoa tatizo kutohudhuria masomo pindi wanapokuwa katika hedhi''
    Dollah Kusenge
    Kasulu
    Mkurugenzi wa Wilaya ya Kasulu
  • 'Hatutaki mtoto wa miaka 6 afikirie kuwa Mwali, afikirie kuchezwa ngoma tunataka afikirie kusafirisha Cherry tomato nje ya nchi' - Mh. Jokate Mwegelo
    Jokate Mwegelo
    Wilaya ya Kisarawe
    Mkuu wa Wilaya

ABOUT US

  • About us
  • Advertise
  • Jobs
  • Terms & Conditions
  • Contact Us
  • Frequently Asked Questions

Network

  • IPP MEDIA
  • EAST AFRICA RADIO
  • ITV
  • RADIO ONE
  • CAPITAL RADIO
  • LOKOPROMO

©  East Africa Television Limited. All Rights Reserved

  • Main menu
    • Home
    • Shows
    • News
      • Currrent Affairs
      • Entertainment
      • Sport
      • Business
      • Life & Style
    • Gallery
    • Schedule
      • Awards
      • BBALLKINGS
      • Dance100
    • Namthamini
  • Search
  • Main menu
    • Home
    • Shows
    • News
      • Currrent Affairs
      • Entertainment
      • Sport
      • Business
      • Life & Style
    • Gallery
    • Schedule
      • Awards
      • BBALLKINGS
      • Dance100
    • Namthamini
  • Search